Serikali itaendeleza jitihada za kuimarisha zao la Pamba kwa kutoa elimu na pembejeo kwa wakulima ili kuleta tija na bei yenye uhalisia kwa manufaa yao na wadau wa mnyororo mzima wa zao hilo.
Amesema Mhe. Daniel Chongolo (Mb), Waziri wa Kilimo wakati wa Mkutano wa Wadau wa Tasnia ya Pamba tarehe 16 Aprili 2026, Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma.