Wadau mbalimbali wa Sekta ya Kilimo wanaotekeleza Programu ya Mifumo Himilivu ya Chakula Tanzania (TFSRP) tarehe 17 na 18 Machi, 2025 wameshiriki mafunzo elekezi ya kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa (Climate Adaption) yaliyotolewa na Benki ya Dunia (WB) kwa kushirikiana na Global Climate Adaption (GCA) katika Ukumbi wa Nashera jijini Dodoma.
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) ikikagua ujenzi wa mradi wa vihenge na maghala ya kisasa vya kuhifadhia mazao vinavyosimamiwa na Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA), wilaya ya Babati, Mkoa wa Manyara
Mradi wa vihenge na maghala ya kisasa kwa ajili ya kuongeza uwezo wa kuhifadhi nafaka unaosimamiwa na Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA)
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo, Mifugo na Uvuvi ikiwa katika ziara Mkoa wa Tabora ya kukagua jengo la kitega uchumi la Ofisi ya Bodi ya Tumbaku tarehe 16 Machi 2025.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo (anayesimamia Ushirika na Umwagiliaji), Dkt. Stephen Nindi akiieleza Kamati ya Kudumu ya Bunge Viwanda, Biashara, Kilimo, Mifugo na Uvuvi kuwa mradi wa umwagiliaji unaogharimu shilingi bilioni 13.6 wa Bwawa la Nyida umefikia asilimia 75% ya utekelezaji wake.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Mweli amekutana kwa mazungumzo na wawakilishi kutoka nchini Zambia wakiongozwa na Waziri wa Kilimo wa Zambia, Mhe. Reuben Phiri tarehe 14 Machi 2025, jijini Dodoma. Viongozi hao wamejadili kuhusu kukuza ushirikiano wa kibiashara wa mauzo ya chakula kati ya nchi hizo mbili.
Mkuu wa Mkoa Simiyu, Mhe. Kenani Kihongosi akitoa taarifa kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo, Mifugo na Uvuvi iliyoambatana na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo (anayesimamia Ushirika na Umwagiliaji), Dkt. Stephen Nindi na Wataalamu kutoka Wizara ya Kilimo wakati wakiendelea na ziara ya kikazi tarehe 12 Machi 2025
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo, Mifugo na Uvuvi wakifanya ziara ya kukagua Kituo Mahiri cha Zana za Kilimo kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Itilima, Mkoani Simiyu tarehe 12 Machi 2025
Wajumbe kutoka Benki ya Dunia na Wataalamu kutoka Wizara ya Kilimo wakiwa katika Kampuni ya IFL (ITRACOM Fertilizers Limited) iliyopo jijini Dodoma, tarehe 12 Machi 2025 wakifanya ziara ya ukaguzi wa utekelezaji wa Programu ya Mifumo Himilivu ya Chakula Tanzania (TFSRP) inayotekelezwa kupitia Wizara ya Kilimo na Taasisi zake.
Wajumbe kutoka Benki ya Dunia wakiongozwa na Bi. Frauke Jungbluth ambaye ni Meneja Kilimo na Chakula katika ukanda wa Kusini na Mashariki ya Afrika wa Benki ya Dunia (Practice Manager Agriculture and Food in Southern and Eastern Africa World Bank) wakifanya ukaguzi wa utekelezaji wa Programu ya Mifumo Himilivu ya Chakula Tanzania (TFSRP) inayotekelezwa kupitia Wizara ya Kilimo na Taasisi zake, tarehe 12 Machi 2025 jijini Dodoma.