Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imewahakikishia wakulima wa Mkoa wa Rukwa kunufaika na miradi ya umwagiliaji thaman iya Shilingi Bilioni 51.9 huku ikiwataka wakulima kuwa makini wanaponunua mbegu za ruzuku kwa kuhakikisha zina lebo ya Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI).
Amesema Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. David Silinde (Mb) wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungamo Tanzania, Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) tarehe 9 Machi 2026, katika Wilaya ya Nkasi, Mkoani Rukwa.